Monday, January 6, 2014
Sunday, January 5, 2014
Self Kuwa Feat. Fleah - Long Time (D.R.C) [Official Music Video]
Sunday, January 05, 2014
No comments
Saturday, December 21, 2013
Saturday, December 14, 2013
Wednesday, December 11, 2013
ZITTO AWASHA MOTO CHADEMA
Siku moja baada ya kuwasilisha maelezo yake ya utetezi baada ya kuvuliwa nyadhifa zake ndani ya Chadema, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe amekata rufaa Baraza Kuu kupinga hatua hiyo.
Zitto pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema
Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila
Mkumbo walivuliwa nyadhifa zao na Kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika
Novemba 20 na 21 jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jana, Mwanasheria wa Zitto, Albert
Msando alitaja sababu mbili za kukata rufaa kuwa ni kukiukwa kwa
taratibu za kuchukua hatua za nidhamu na sababu zilizotolewa kutokuwa
sahihi.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa
Chadema, John Mnyika alisema mambo hayo yalishatolewa ufafanuzi na chama
na kwamba kukata rufaa ni haki ya kikatiba kwa mwanachama yeyote.
“Kukata rufaa ni haki
ya kikatiba ya wanachama yeyote. Rufaa ikatwe tu, itashughulikiwa kwa mujibu wa katiba, kanuni, maadili na itifaki ya chama. Hata hivyo, ieleweke, rufani inahusu kuvuliwa nafasi za uongozi, kusudio hilo haliwaondolei wajibu wa kujieleza kwa maandishi mbele ya Kamati Kuu kwa nini wasifukuzwe uanachama,” alisema Mnyika.
ya kikatiba ya wanachama yeyote. Rufaa ikatwe tu, itashughulikiwa kwa mujibu wa katiba, kanuni, maadili na itifaki ya chama. Hata hivyo, ieleweke, rufani inahusu kuvuliwa nafasi za uongozi, kusudio hilo haliwaondolei wajibu wa kujieleza kwa maandishi mbele ya Kamati Kuu kwa nini wasifukuzwe uanachama,” alisema Mnyika.
Sababu za kukata rufaa
Akifafanua sababu za kukata rufaa, Msando alitaja
kifungu cha 6.5.6 cha Kanuni ya Uendeshaji ya chama hicho, akisema
utaratibu uliotakiwa kufuatwa kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu
kiongozi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni ni kupewa kwanza mashtaka kwa
maandishi ili apate nafasi ya kujibu.
“Kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu
bila kwanza kupewa mashtaka yake kwa maandishi na mamlaka husika na
kupewa nafasi ya kujibu mashtaka kwa maandishi,” alisema na kuongeza:
“Kwa mujibu wa ibara ya 5.4.3 na 5.4.4 ya Katiba
mwanachama yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama
kuachishwa ama kufukuzwa uanachama bila kujulishwa makosa yake kwa
maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili.”
Alitaja vipengele vingine ni kupewa nafasi ya
kujitetea mbele ya kikao kinachohusika na atajulishwa kwa maandishi
uamuzi wa kikao ndani ya wiki mbili baada ya kusikilizwa.
Hata hivyo, kipengele ‘d’ kinasema: “Kamati Kuu
inaweza kuchukua hatua za dharura bila kuzingatia utaratibu (b), (c)
hapo juu kama itaona masilahi ya chama kwa ujumla yanaweza kuathiriwa
isipokuwa mwanachama au kiongozi anayelalamikiwa atalazimika kuitwa
kwenye kikao husika.
Alifafanua kuwa, siku ya kikao cha Kamati Kuu,
Zitto hakupewa mashtaka yake bali aliyakuta ndani ya kikao baada ya
kupewa taarifa kwa ujumbe wa simu (text message au sms). Zitto hakuwepo
katika mkutano wa jana na waandishi wa habari.
“Kwa uzito wa makosa hayo yaliyosababisha kuvuliwa uongozi na
kwa kuangalia athari zake kwake yeye binafsi na chama kwa jumla, Kamati
Kuu ilitakiwa kujiridhisha kwamba kanuni za uendeshaji na katiba
zinafuatwa,” alisema.
Mbali na Zitto, Msando alisema makosa hayo pia
yalifanyika kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha,
Samson Mwigamba. “Yeye hakuitwa kabisa kwenye kikao hicho na ni
ukiukwaji wa Kanuni ya Uendeshaji 6.5.6(d),” alisema.
Aliongeza kuwa hata waraka wa mabadiliko ulioelezwa kuwa sababu ya Zitto kupewa adhabu hiyo haumtaji kabisa.
Akieleza nia ya Zitto kukata rufaa, Msando alinukuu katiba ya chama hicho ibara 6.3.6(d) na ibara 6.3.6(e) akisema:
“Kiongozi aliyechukuliwa hatua za kinidhamu na
mamlaka yake ya nidhamu anayo haki ya kukata rufaa ngazi ya juu ya ile
mamlaka yake ya nidhamu na uamuzi wa ngazi hiyo utakuwa wa mwisho”,”
alisema na kuongeza:
“Huo ndio utaratibu ambao Zitto Kabwe ameamua
kufuata kwa kuheshimu maamuzi ya Kamati Kuu lakini kukatia rufaa maamuzi
hayo. Kuheshimu maamuzi siyo kuyakubali uhalali wake.”
Akana kuhujumu ziara ya Dk Slaa Kigoma
Katika hatua nyingine Msando alisema kuwa matukio
ya vurugu yanayoiandama ziara ya Katibu Mkuu wa chama hicho mkoani
Kigoma hayana uhusiano wowote na Zitto.
“Zitto Kabwe hahusiki kwa njia yoyote na hayo
yanayoendelea na anayakemea na kuwashauri wanachama wote kuwa watulivu
na kuendelea kuwaheshimu viongozi wa kitaifa,” alisema Msando.
TOP 5 YA VICHEKESHO VYA VUNJA MBAVU HIVI HAPA...SOMA UCHEKE HADI BASII NI NOMAAA.
- Jamaa aliamua kumtoa demu wake out kwa ajili ya chakula cha usiku kufika hotelini wakakaa mezani muhudumu akaja,kaka nikuhudumie nini, tafadhali:NILETEE MENU LIST: dada na wewe,dada akajibu kwa pozi tena kwakujishaua,"NA MIMI NILETEE MENU LIST ILA CHUMVI WEKA KWA MBAAAAALI!
- Hii Ni Kweli Ilitokea mitaa Fulani..na hata Ukicheki Sikuhizi wanaume huwa wanaendesha hovyo sana wanapoona wanawake wazuri/warembo mbele yao..
- Ukikutana na Mwanamke mtata na ukamfanyia Upuuzi au Masihara Lazima Ujute maana Utapigwa Mangeu kama Huyu jamaa hapo chini... ni shidaaa
- Ukitaka kujua mwanamke sio ndugu yako soma hii hapa upate undani. Jamaa karudi toka job mpole!
MUME: ofisi yetu imeungua na watu wote wamekufa,
MKE: ilikuwaje wewe ukapona?
MUME: nilikuwa chooni, jirani na ofisi najisaidia.
MKE: Loh masikini familia zao itakuwaje?
MUME: watalipwa milioni 100 kila mfiwa.
MKE KWA HASIRA: ona sasa na wewe kunya kunya kwako umetukosesha mihela..ungeenda kunya akhera......
Ungekuwa Mwanaume Ungejibu Vip ?
- DOGO KAULIZWA SWALI NA BABA YAKE Huku kaweka Sura ya Tabasamu...akajibu Ujinga....BABA alipogeuka na KUKAZA sura DOGO akarekebisha Kauli Ili yasimpate Mabaya...Nomaa Sana.. WAzazi Inabidi Kuwa Wakali Mara Nyingne...
Sunday, December 8, 2013
MWANAMUME AKIKOSA MTOTO HUPATA HUZUNI ZAIDI KULIKO MWANAMKE
Tofauti na mazoea na mtazamo wa wengi kwamba mwanamke ndiye anayeumia zaidi akikosa mtoto, wataalamu wamegundua kuwa anayeumia zaidi kwa kukosa mtoto ni mwanamume.
Utafiti huo umeonyesha kuwa wanaume wanahitaji mtoto sawa sawa na wanavyohitaji wanawake, lakini wao wanaumia zaidi wanapokosa bahati ya kupata mtoto.
Wataalamu hao wamebaini kuwa sababu kubwa
zinazowafanya wanaume wajisikie vibaya zaidi wanapokosa watoto ni
tamaduni za toka enzi kuwa wao wanaweza kila kitu na msukumo wa familia.
Tofauti na wanawake, ambao wanahitaji mtoto kwa
ajili yao binafsi kwa asili ya kuumbwa kwao, hali ambayo kitaalamu
inajulikana kama ‘biological urge’.
Taarifa za utafiti huo ulioongozwa na Robin
Hadley, wa Chuo Kikuu cha Keele, ukishirikisha wanaume 27 na wanawake
81, ambao hawajapata mtoto, uliwasilishwa mbele ya Wanasaikolojia wa
Taasisi ya British Sociological Association, ya Uingereza.
Waohitaji zaidi watoto
Kwa idadi hiyo waliosema wanahitaji watoto ni wanaume asilimia 59 na wanawake ni asilimia 63.
Nusu ya wanaume walisema kukosa mtoto kunawafanya waonekane tofauti kwenye jamii, huku wanawake wakisema wanahitaji watoto ili waje kuwasaidia baadaye.
Kwa idadi hiyo waliosema wanahitaji watoto ni wanaume asilimia 59 na wanawake ni asilimia 63.
Nusu ya wanaume walisema kukosa mtoto kunawafanya waonekane tofauti kwenye jamii, huku wanawake wakisema wanahitaji watoto ili waje kuwasaidia baadaye.
Utafiti huo ulibaini kuwa asilimia 38 ya wanaume
walihitaji mtoto kwa kuwa hawakuwa na mtoto kabisa, huku asilimia 27 tu
ya wanawake ndiyo walikuwa hawana watoto kabisa.
Utafiti mwingine ulionyesha kuwa wanaume
wanajisikia vibaya zaidi kukosa watoto kwa sababu asilimia ya wasio na
watoto ni wanaume,tofauti na wanawake ambao wakati mwingine hubahatika
kupata mmoja au wawili.
Tafiti hizo zilionyesha kuwa kati ya kila wanaume
wanne mmoja hana kabisa mtoto ikilinganishwa na asilimia 18 ya wanawake
ambao hawana watoto.
Utafiti mwingine ulionyesha kuwa asilimia 56 ya
wanaume hawana watoto kabisa, ikilinganishwa na asilimia 43 ya wanawake
ambao hawana.
Akizungumzia utafiti wake Dk Hadley, anaeleza
kwamba amegundua kuwa kati ya wazazi wawili aliye kwenye hatari ya
kukosa mtoto kabisa ni mwanaume, huku akiumia zaidi anapopatwa na hali
hiyo kiasi cha kuwa na hasira, kujisikia vibaya mbele za watu, kujitenga
na jamii, kuwa na wivu na mambo yanayofanana na hayo.
Wanawake kupenda watoto
Anabainisha kuwa hiyo ndiyo sababu inayowafanya wanawake wapende kupata watoto kuliko wanaume ili kuwaondoa kwenye matatizo hayo, ambayo mara nyingi husababisha familia nyingi kusambaratika bila kujali zilikuwa kwenye maelewano ya kiasi gani.
Anabainisha kuwa hiyo ndiyo sababu inayowafanya wanawake wapende kupata watoto kuliko wanaume ili kuwaondoa kwenye matatizo hayo, ambayo mara nyingi husababisha familia nyingi kusambaratika bila kujali zilikuwa kwenye maelewano ya kiasi gani.
Alisema kwamba utafiti huo ulifanyika kwa njia ya
kukusanya maoni kwenye mtandao, midahalo, kujaza dodoso za majibu na
ulihusisha watu wenye umri wa kati ya miaka 20-66 huku wengi waliojibu
maswali hayo walikuwa na umri usiopungua miaka 41.
Subscribe to:
Posts (Atom)